Thursday, June 28, 2012

Ngoma zetu
Kama ilivyo kwa jadi zote. Wanyisanzu wana ngoma ambazo huchezwa katika matukio mbalimbali ya kijamii kama harusi n.k. Ngoma kuu inajulikana kama "Nki'ninta" hii huchezwa na wanaume na wanawake rika zote. Hujipanga mistari miwili wakitizamana na wanaume huruka kwa mirindimo maalumu wanawake hutingisha mabega. 

Njuga au Nkinda kwa kinyisanzu hutumika kwa kuvaliwa miguuni nazo hutoa milio pia. pia kuna mbutu ambazo hutumika zaidi kwa shughuli za dini za asili yaani wapagani. Mbutu ni bomba kama pembe ndefu ambazo hupulizwa na kutoa mlio. Wapiga mbutu waliweza kutambulika kwa kuwa midomo yao ilibadilika rangi na kuwa pink. Nitawaletea habari zaidi. (Kwa hisani ya simulizi ya ndugu na jamaa)
Vyakula vikuu vya Wanyisanzu
Vyakula vya asili vya Wanyisanzu ni ugali wa mtama ukiambatana na mboga ya mlenda wa kusaga(Ndalu) au fresh, au mboga mbali mbali za kijani zilizokaushwa kama nsansa, nsonga, kwa kawaida nyama hukaushwa na kuwekwa chumvi ikijulikana kama "mintanda" Vyakula hivi husindikizwa na maziwa ya mtindi. 

Kwa upande wa matunda, kabila hili lilitegemea zaidi matunda ambayo si kutoka bustanini ila matunda yaliojiotea yenyewe kama matogo, mbura,furu, nsalati, nkuyu, ngumo, ntundwa, lade, matini n.k. Wenyeji pia hupendelea kunywa togwa ya unga wa mtama na pombe za kienyeji.

Hapo zamani hakukuwa na mashine za kusaga nafaka, mawe yalichongwa na kuitwa Lwala (jiwe kubwa) na dogo (Nsio) hivi vinatumika kusaga nafaka. kwa baadhi ya maeneo bado hutumia haya mawe kusaga nafaka. Nitaendelea kuelezea zaidi na kuweka taswira nitakapotembelea huko na kupewa habari zaidi.  (chanzo ni simulizi toka kwa ndungu mbali mbali). Asante Aunt Frida Mzengi na Uncle Paulo Mtiko kwa michango yenu.
                                                              Mlenda wa kusaga (Ndalu).